Thursday, August 7, 2025

TADB Yawezesha mapinduzi ya uvuvi na ufugaji wa samaki nchini: Kutoka Uvuvi wa Kujikimu Hadi Uchumi Endelevu kwa Vijana na Wavuvi Wadogo

 

Ufugaji wa Samaki Ndani ya Vizimba (Cage Farming)

Uvuvi wa Kisasa na Ufugaji wa Samaki Wakua Kiuchumi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imekuwa kinara wa mapinduzi katika sekta ya uvuvi na ufugaji wa samaki. Kupitia mikopo nafuu na ya kimkakati, TADB imefungua milango ya uchumi kwa wavuvi wadogo, vijana na wakulima wa maji nchini.

Uvuvi wa Kisasa kwa Mashua za Kisasa

Kwa kutoa zaidi ya TZS bilioni 14.23, TADB imefadhili ununuzi wa boti 190, na kuwawezesha wavuvi wadogo 3,329 katika mikoa 16 kubadili maisha yao kutoka uvuvi wa kujikimu hadi kibiashara. Mafanikio haya yamechochea:

  • Thamani ya mazao kuongezeka kupitia huduma za baridi na uchakataji wa samaki.

  • Ajira mpya kupitia wauzaji wa vifaa, mafundi na wauza samaki.

  • Wavuvi wengi kuingia rasmi katika mfumo wa kifedha—wengi wao wakiwa hawakuwa na akaunti awali.

Ufugaji wa Samaki Ndani ya Vizimba (Cage Farming)


Katika Kanda ya Ziwa, ambapo uvuvi wa jadi unakabiliwa na upungufu wa samaki pori, TADB ilikuja na suluhisho bunifu: ufugaji wa samaki ndani ya vizimba. Kupitia mikopo ya TZS bilioni 8.36, TADB imewezesha:
  • Ujenzi wa vizimba 337.

  • Wakulima wa maji 1,631 kufaidika, ikiwemo vijana 1,223.

Mafanikio haya yameleta mabadiliko ya kweli:

  • Samaki zaidi ya tani  2,651.8 zimevunwa, na kuchangia TZS bilioni 2 kwenye uchumi wa mikoa.

  • Familia zimeanza kupata kipato cha uhakika na maisha bora.

  • Vikundi 25 vililipa mikopo yao ya awali na kupewa tena mikopo kwa awamu ya pili.

  • Vijana waliowezeshwa ni asilimia 75 ya walionufaika na ufugaji huu wa kisasa.

Takwimu Muhimu:
  • 💸 TZS Bilioni 8.36 – Fedha zilizotolewa kwa ajili ya ufugaji wa samaki Kanda ya Ziwa

  • 🛖 Vizimba 337 – Vimejengwa kwa wakulima wa maji

  • 🧑🏽‍🌾 Vijana 1,223 – Wamepata ajira kupitia ufugaji wa samaki

TADB: Benki ya Mabadiliko ya Kilimo Tanzania

 

Bagamoyo Sugar

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ni taasisi ya kifedha ya serikali iliyoundwa rasmi mwaka 2015 kwa lengo maalum kuchochea mageuzi ya sekta ya kilimo nchini kupitia mikopo ya muda mrefu, nafuu na jumuishi.

Kwa miaka 10 sasa, TADB imekuwa kinara wa mapinduzi ya kifedha katika kilimo. Imewezesha wakulima zaidi ya 1.9 milioni, mashirika ya wakulima, na biashara za kilimo kufikia zaidi ya TZS trilioni 1.1 kupitia mikopo ya moja kwa moja, dhamana za mikopo, na ushirikiano na taasisi za fedha.

Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania, lakini kilikuwa kinakabiliwa na changamoto kama ukosefu wa mitaji, miundombinu duni, na kutengwa kwa wakulima wadogo—hasa wanawake na vijana. TADB ilianzishwa kama jibu la kitaifa kwa pengo hilo la kifedha, ikilenga kuchochea uzalishaji wa chakula, usalama wa chakula, na maendeleo ya viwanda vya kuchakata mazao.

Kwa sasa, TADB ni benki ya daraja la kwanza (Tier 1), ikiwa na mtaji mkubwa, mifumo ya kisasa ya kidigitali, na mipango bunifu kama Mfumo wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo (SCGS) ambao umesaidia kuvutia taasisi za fedha binafsi kuwekeza katika kilimo.

Kupitia uwekezaji wake, TADB si tu kwamba imeongeza uzalishaji wa mazao kama mpunga, miwa, kahawa, na pamba, bali pia imekuwa sehemu ya mkakati wa taifa wa kuhakikisha Tanzania inajitosheleza kwa chakula na kuwa kitovu cha usambazaji Afrika Mashariki.

TADB Yawezesha mapinduzi ya uvuvi na ufugaji wa samaki nchini: Kutoka Uvuvi wa Kujikimu Hadi Uchumi Endelevu kwa Vijana na Wavuvi Wadogo

  Ufugaji wa Samaki Ndani ya Vizimba (Cage Farming) Uvuvi wa Kisasa na Ufugaji wa Samaki Wakua Kiuchumi  Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzan...